Breaking


Jumamosi, 5 Septemba 2026

LAMINE YAMAL AONGEZWA KWENYE KUNDI LA MANAHODHA WA BARCELONA




Barcelona, Hispania 


Winga wa FC Barcelona, Lamine Yamal, ameongezwa kwenye kundi la manahodha wa timu hiyo baada ya kupigiwa kura na wachezaji wenzake ndani ya kikosi.

Uamuzi huo unamfanya Yamal kuwa miongoni mwa wachezaji watano wanaounda kundi la manahodha wa Barcelona, akijiunga na Raphinha, Pedri, Frenkie de Jong na Eric García.

Yamal, ambaye bado ana umri wa miaka 19, sasa anakuwa sehemu ya uongozi wa kikosi cha Barcelona, hatua inayompa nafasi kubwa zaidi katika majukumu ya ndani ya timu.



Kuongezwa kwake kwenye kundi hilo pia kunaonyesha kuongezeka kwa imani kutoka kwa wachezaji wenzake, huku akiwa miongoni mwa wachezaji vijana wanaopewa jukumu la uongozi katika historia ya klabu hiyo.

Kwa mujibu wa taarifa hizo, uteuzi huo umefanyika kufuatia mchakato wa upigaji kura wa ndani wa wachezaji wa Barcelona.


Hakuna maoni: