Liverpool wako tayari kutoa ofa itakayovunja rekodi ya uhamisho Uingereza kwa mshambuliaji wa Newcastle na Sweden Alexander Isak, 25 (Mail+).
Lakini klabu ya Saudi Al-Hilal pia wanajiandaa kutoa ofa, inayodhaniwa kuwa zaidi ya pauni milioni 130, kwa Isak baada ya kuondolewa kwake kwenye kikosi cha Newcastle kilichoko kwenye ziara yao ya maandalizi ya msimu mpya huko Singapore (Talksport).
Chelsea na Manchester United hawana uwezekano wa kumsajili Isak, huku United wakiwa tayari wametumia fedha nyingi kuwasajili mshambuliaji wa Brazil Matheus Cunha, 26, na mchezaji wa kimataifa wa Cameroon Bryan Mbeumo, 25 (Mail).
Newcastle wameelekeza mawazo yao kwa mchezaji wa kimataifa wa Slovenia Benjamin Sesko huku mshambuliaji huyo wa RB Leipzig mwenye umri wa miaka 22 akiwa mbadala iwapo Isak ataondoka (ipaper).
Aston Villa wameiambia Manchester United kuwa mshambuliaji Ollie Watkins hauzwi, licha ya klabu hiyo ya Old Trafford kumtaka sana mchezaji huyo wa Kiingereza mwenye umri wa miaka 29 (Telegraph).

Hakuna maoni:
Chapisha Maoni