Breaking

Ijumaa, 11 Julai 2025

TUENDELEE KUSAMBAZA VIELELEZO VYA ELIMU YA AFYA KATIKA MAENEO YETU-DKT. MACHANGU


Mkurugenzi Msaidizi wa Elimu ya Afya kutoka  Wizara ya Afya Dkt.Ona Machangu ametoa wito  kwa jamii  kuendelea kushirikiana na Serikali katika usambazaji wa vielelezo vya elimu ya Afya ikiwemo shuleni na masokoni vinavyozalishwa na Wizara ya Afya.

Dkt. Machangu ametoa wito huo leo  Julai 11, 2025  Jijini Dodoma, wakati akiwasilisha wasilisho la Elimu ya Afya  kwenye Mkutano wa Mwaka wa Waganga Wakuu wa Mikoa na Halmashauri .

"Moja ya majukumu ya Elimu ya Afya kwa Umma ni kuzalisha vielelezo vyenye maudhui ya elimu ya afya, hivyo niwaombe vielelezo vinaposambazwa katika maeneo mbalimbali kila mmoja ana wajibu wa kuvisambaza vielelezo hivyo," amesema Dkt. Machangu.

Aidha, Dkt. Machangu amesema suala la elimu ya Afya isiwe kwenye masuala ya dharura tu, hivyo ni muhimu kuwa endelevu.

Halikadhalika, Dkt. Machangu amesema elimu ya afya kwa umma imekuwa ikitumia namba namba 199 kwa kupokea maoni ya wananchi kuhusu masuala mbalimbal

Hakuna maoni: