Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetoa angalizo la uwezekano wa kutokea mvua kubwa katika maeneo machache ya Mkoa wa Ruvuma, kuanzia leo Ijumaa Februari 06 hadi Jumanne Februari 10, 2026.
Kwa mujibu wa taarifa ya TMA iliyotolewa leo saa 9:30 mchana, mvua hizo zinatarajiwa kuwa na uwezekano wa kutokea kwa kiwango cha wastani, huku athari zake pia zikitajwa kuwa za kiwango cha wastani.
🌧️ Athari Zinazoweza Kujitokeza
TMA imeeleza kuwa miongoni mwa athari zinazoweza kujitokeza ni pamoja na:
- Baadhi ya makazi kuzungukwa au kujaa maji
- Changamoto za muda mfupi katika shughuli za kijamii na kiuchumi
Kutokana na hali hiyo, wananchi wametakiwa kuzingatia tahadhari na kujiandaa mapema ili kuepuka madhara yanayoweza kusababishwa na mvua hizo.
📅 Matarajio ya Siku Tano
- Ijumaa, 06/02/2026: Angalizo la mvua kubwa – Tahadhari ya wastani
- Jumamosi, 07/02/2026: Hakuna tahadhari
- Jumapili, 08/02/2026: Hakuna tahadhari
- Jumatatu, 09/02/2026: Hakuna tahadhari
- Jumanne, 10/02/2026: Hakuna tahadhari
TMA imesisitiza kuwa itaendelea kufuatilia mwenendo wa hali ya hewa na kutoa taarifa zaidi endapo kutakuwa na mabadiliko.



Hakuna maoni:
Chapisha Maoni