Akizungumza kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) katika Mkutano wa Mwaka wa Tanzania wa Anwani za Makazi 2026, Mkurugenzi Mkuu wa TCRA, Jabir Mohamed, amesema suala la anwani za makazi sasa ni ajenda ya kimkakati ya taifa, hasa katika kipindi hiki cha ukuaji mkubwa wa uchumi wa kidijitali.
Kwa upande wake, akizungumza kwa niaba ya Postmaster Mkuu wa Shirika la Posta Tanzania (TPC), Kaimu Mkurugenzi wa Masoko na Mauzo, Ferdinand Kabyamela, amesema Mfumo wa Taifa wa Anwani za Makazi umeirahisishia jamii ya wafanyabiashara kujisajili rasmi, kupata huduma za kibenki, mikopo na bima kwa urahisi zaidi.

Hakuna maoni:
Chapisha Maoni