Hali hiyo ilimgusa sana mwalimu wake, Miss Roberts, ambaye kwa ukimya na upendo alimnunulia viatu ili kumrejeshea heshima na kujiamini darasani. Kilikuwa kitendo kidogo, lakini chenye maana kubwa sana katika maisha ya mtoto huyo.
Miaka ilivyopita, Rihanna alikua na kuwa nyota mkubwa wa kimataifa, akitawala muziki na biashara duniani. Hata hivyo, hakusahau alikotoka wala watu waliogusa maisha yake.
Alipogundua kuwa mwalimu wake huyo alikuwa akipitia wakati mgumu kimaisha, aliamua kumshukuru kwa namna ya kipekee. Rihanna alimzawadia nyumba pamoja na msaada wa kifedha wa kila mwezi.
Ni simulizi inayotukumbusha kuwa wema mdogo unaweza kubadilisha maisha ya mtu milele. Kweli kabisa, fadhila haiozi.

Hakuna maoni:
Chapisha Maoni