Rais wa Urusi, Vladimir Putin, anasafiri kwenda China kukutana na kiongozi wa China, Xi Jinping, ikiwa ni chini ya wiki moja baada ya Rais wa Marekani, Donald Trump kukamilisha ziara yake mjini Beijing.
Putin amepangwa kuwa nchini China leo na kesho katika ziara ambayo huenda ikafuatiliwa kwa karibu wakati China ikijitahidi kudumisha uhusiano thabiti na Marekani na wakati huo huo pia ikidumisha uhusiano imara na Urusi.
Ikulu ya Kremlin imesema Putin na Xi wanapanga kujadili ushirikiano wa kiuchumi kati ya nchi hizo mbili, lakini pia "masuala muhimu ya kimataifa na kikanda."
Ziara hiyo inaambatana na maadhimisho ya miaka 25 ya Mkataba wa Urafiki kati ya China na Urusi uliosainiwa mwaka wa 2001.
Putin alizuru China mara ya mwisho mwezi Septemba mwaka 2025 kuhudhuria mkutano wa kilele wa kila mwaka wa Jumuiya ya Ushirikiano ya Shanghai huko Tianjin, kutazama gwaride la kijeshi linaloadhimisha kumbukumbu ya miaka 80 ya kumalizika kwa Vita vya Pili vya Dunia na kufanya mazungumzo na Rais Xi.

Hakuna maoni:
Chapisha Maoni