Breaking


Alhamisi, 13 Agosti 2026

SELEMANI MWALIMU AANZA SAFARI YANGA SC KWA KUNYAKUA NGAO YA JAMII 2026


Usajili wa Selemani Mwalimu kutoka Simba SC kwenda Yanga SC ulizua mjadala mkubwa katika ulimwengu wa soka nchini Tanzania. Hata hivyo, nyota huyo tayari ameanza safari yake mpya akiwa na taji la kwanza akiwa upande wa Jangwani.


Yanga SC imeifunga Simba SC kwa bao 1-0 na kutwaa Ngao ya Jamii 2026 katika mchezo uliokuwa na ushindani mkubwa. Bao pekee la mchezo lilifungwa na Albert Kangwanda, na kuiwezesha Yanga SC kuibuka na ushindi pamoja na taji.


Kwa upande wa Selemani Mwalimu, ushindi huo unamfanya kuanza kipindi chake kipya Yanga SC akiwa tayari ameshuhudia timu yake ikitwaa taji.

Selemani Mwalimu: Kombe 1 | Simba SC: 0

Ushindi huo unaongeza hamasa kuelekea msimu mpya wa soka, huku mashabiki wa Yanga SC wakitarajia kuona mchango wa Selemani Mwalimu katika safari ya timu hiyo kwenye mashindano mbalimbali.


Hakuna maoni: