Breaking


Ijumaa, 11 Septemba 2026

SALAMU ZA POLE NA RAMBIRAMBI – SEKTA BINAFSI TANZANIA 🇹🇿

Kiongozi wa Sekta Binafsi Tanzania na Mmiliki wa Bravo Group na Agricom, Bi. Angelina Ngalula, amefikisha salamu za pole na rambirambi kwa Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kufuatia msiba wa kuondokewa na mwenza wake mpendwa, Mhe. Maalim Hafidh Ameir Hassan


Bi. Ngalula alifika kwa niaba ya Sekta Binafsi Tanzania, akiwa ameambatana na Mkurugenzi wa Sera na Utafiti wa TPSF, kuwasilisha pole kwa niaba ya wadau wote wa Sekta Binafsi walioshindwa kufika binafsi


Tunamuomba Mwenyezi Mungu amuweke Marehemu mahali pema peponi, na awape Mhe. Rais, familia na ndugu wote subira na faraja katika kipindi hiki cha majonzi.


*Innā lillāhi wa innā ilayhi rājiʿūn. 🇹🇿*


#TPSF #SektaBinafsiTanzania #SalamuZaPole #Rambirambi

Hakuna maoni: