Breaking


Jumanne, 8 Septemba 2026

WACHEZAJI 30 WATANGAZWA KUIWANIA TUZO YA BALLON D’OR 2026



Wachezaji 30 wametajwa katika orodha ya wanaowania tuzo ya
Ballon d’Or 2026, inayotolewa kwa mchezaji bora wa soka duniani.

Orodha hiyo imetangazwa leo kupitia ukurasa rasmi wa Ballon d’Or, huku baadhi ya majina makubwa katika soka la dunia yakijumuishwa kwenye kinyang’anyiro hicho.

Miongoni mwa wachezaji waliotajwa ni Kylian Mbappé, Lamine Yamal, Ousmane Dembélé na Erling Haaland.


Majina mengine ni
Jude Bellingham, Lionel Messi, Vinícius Jr., Harry Kane, Rodri na Vitinha, ambao pia wanatajwa kuwa miongoni mwa wachezaji wanaowania tuzo hiyo yenye heshima kubwa katika soka duniani.

Mshindi wa Ballon d’Or 2026 atapatikana baada ya mchakato wa upigaji kura unaohusisha waandishi wa habari kutoka nchi mbalimbali duniani.


Hakuna maoni: