Barcelona wako tayari kuingia kwenye kinyang'anyiro cha kumsajili beki wa Crystal Palace na Uingereza Marc Guehi kwa uhamisho wa bila malipo msimu ujao huku Liverpool na Real Madrid wakiwa tayari wanamtaka mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25. (Sport - In Spanish)
Beki wa Liverpool Joe Gomez, 28, alivutiwa na Crystal Palace na Brighton siku ya mwisho ya dirisha la uhamisho lakini mchezaji huyo wa kimataifa wa Uingereza alibaki Anfield huku mabingwa hao wa Premier League wakishindwa katika jitihada zao za kumnunua Guehi. (Football Insider,)
Hatima ya beki wa kati wa Uingereza James Tarkowski, 31, beki wa pembeni wa Ukraine Vitalii Mykolenko, 26, na kiungo wa kati wa Uingereza James Garner, 24, itaangaliwa Everton, huku watatu hao wakiwa wameingia miezi 12 ya mwisho ya kandarasi zao. (Times - Subscription Required)
Manchester United wanaweza kurejea kumnunua kiungo wa kati wa Brighton Carlos Baleba mwaka ujao baada ya kushindwa katika jaribio lao la kumsajili mchezaji huyo wa kimataifa wa Cameroon mwenye umri wa miaka 21 katika dirisha la usajili la majira ya kiangazi. (GiveMeSport)
Fulham watatoa kandarasi iliyoboreshwa zaidi kwa Rodrigo Muniz baada ya kumshikilia fowadi huyo wa Brazil mwenye umri wa miaka 24 licha ya kutakiwa na klabu ya Serie A Atalanta msimu wa joto. (GiveMeSport,)
#ChanzoBbcswahili


Hakuna maoni:
Chapisha Maoni